Pambazuko FM Radio
Pambazuko FM Radio
17 July 2025, 7:03 pm

Upelelezi zaidi wa kisayansi unaendelea kuhusiana na utambuzi vinasaba vya wanyama hawa maeneo ambayo wanyama wamepatikana
Na Katalina Liombechi
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na maofisa wa wanyamapori wilaya ya Ulanga limefanikiwa kuwakamata watu wawili wakazi wa kijiji cha Isongo wakiwa na meno 6 ya Tembo.
Watuhumiwa hao ni Televaeri Paranjo 47 mkazi wa kijiji cha Isongo na Freddy Maxmilian Magumba 42 mkazi wa kijiji cha Isongo wamekamatwa julai 14,2025 majira ya asubuhi katika kitongoji cha korowa kijiji na kata ya Isongo Wilaya ya ulanga wakiwa pembeni mwa barabara ya mahenge mwaya.
Kwa mujibu wa kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa wa Morogoro Alex Mkama akizungumza na waandishi wa habari hii leo Julai 17,2025 akiwa Ifarara Wilayani Kilombero amesema kukamatwa kwa watuhumiwa hao ni baada ya taarifa fiche zilizotolewa na wananchi walio wema wanaoishi pembezoni mwa hifadhi huku wakiomba ushirikiano zaidi kutoka kwa wananchi kuhusu watu wanaojihusisha na vitendo hivyo kinyume cha sheria.

Aidha ametoa wito kwa wananchi hasa wanaoishi jirani na maeneo ya Hifadhi kuendelea kutoa ushirikiano wa vitendo vya uhalifu wa namna hiyo,huku akieleza kuwa wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo na kwamba upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani.