Pambazuko FM Radio

Walemavu wasioona kilombero wakumbukwa

22 February 2025, 7:43 pm

Baadhi ya walemavu wasioona wakisubiri msaada wa fimbo nyeupe(Picha na Elias Maganga)

Sisi Watu wenye ulemavu kwa muda mrefu hatujakumbukwa ila tunashukuru kwa huyu mdau Issa Vitus Lipagila kwa kutushika mkono sasa tutafanikisha  shughuli zetu kwa kuepuka  kupata ajali zisizokuwa za lazima[“Walemavu wasioona

Na Elias Maganga

Walemavu wasioona Kilombero wamepatiwa msaada wa fimbo nyeupe 50uliogharimu Tsh,1,500,000/=kutoka kwa mdau Issa Vitus Lipagila ambazo zitawawezesha kutembea ili waweze kufanikisha  shughuli zao kwa kuepuka  kupata ajali zisizokuwa za lazima.

Msaada huo umetolewa baada ya uongozi wa chama cha wasioona Wilaya ya Kilombero kupitia katibu wake Bwana Donath Tulutulu  kumwandikia barua ya maombi ya fimbo nyeupe  50  February 3 mwaka huu ambapo pia mbali na kumshukuru wamemuomba awasidie wapate ofisi ya chama chao,huku Mwenyekiti wa cha cha wasioona Wilaya ya Kilombero Bwana Ismail limbega amewaomba wananchi kwa ujumla wasiuhusishe msaada huo na masuala ya kisiasa kwani msaaada huo ni upendo wa mdau huyo kwa walemavu wasioona .

Katibu wa Chama cha Wasioona Wilaya ya Kilombero Bwana Donath Tulutulu(Picha na Elias Maganga)
Donath Tulutulu na Mwenyekiti wa TLB Kilombero Bwana Ismail Limbega

Akizungumza na walemavu wasioona febr22,2025 katika shule ya msingi Ifakara wakati akiwapatia walemavu hao fimbo 50 Bwana Issa Vitus Lipagila amesema mahitaji yote waliyoyaomba ya kupata jengo la ofisi na kufanya kampeni ya kupita nyumba kwa nyumba ili kuwabaini walemavu ambao baadhi inadaiwa mpaka sassa bado wanafungiwa ndani.

Amesema kampeni ya kupita nyumba kwa nyumba ili kuwabaini walemavu ambao baadhi inadaiwa mpaka sassa bado wanafungiwa ndani inaanza mapema huku upatikanaji wa uwanja na ujenzi wa ofisi ukifanyiwa kazi mara moja

Mdau Issa Vitus Lipagila aliyevaa T-shirt ya mikono mirefu(Picha na Elias Maganga)
Sauti ya Issa Vitus Lipagila

Baadhi ya walemavu waliopatiwa msaada wa fimbo nyeupe wamemshukuru mdau huyo na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kuwasidia kwani walemavu wana mahitaji mengi ambayo jamii kwa ujumla inatakiwa kuwajali kwani walemavu ni watu kama walivyo wengine

Bwana Issa Lipagila akimpatia fimbo nyeupe mlemavu asiyeona Mwalim Janet Kalulu(Picha na Elias Maganga)
Sauti za baadhi ya walemavu

Rais Dr Samia Suluh Hassana anaingia madarakani alikaa na walemavu nchi nzima jijini Dodoma na kuzungumza nao

Hiyo ni ishara ya kuonyesha upendo katika kundi hilo.