Boma Hai FM

Wananchi watakiwa kutunza mazingira kwa kupanda miti

27 January 2026, 4:43 pm

Pichani ni Diwani wa kata ya Machame magharibi Mhe. Martin Munisi akipanda miti (Picha na vivian kweka)

Machame Magharibi wameadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupanda miti pembezoni mwa Barabara kata ya Machame Magharibi

Na Vivian Kweka, Hai-Kilimanjaro

Diwani wa kata ya Machame Magharibi  Martin Munisi amewataka wananchi kuacha kukata miti hovyo na  badala yake wafuate vibali vinavyotolewa na mamlaka husika kwani kumekua na tabia ya baadhi ya wananchi kukata miti hovyo na kusababisha uharibifu wa mazingira.

Ameyasema hayo  Januari 27 ,2026 wakati akiongoza wananchi kupanda miti mia tano kwenye eneo la hifadhi ya barabara katika kuadhimisha siku kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwamba wananchi  wameshiriki kikamilifu katika shughuli hiyo, wakionyesha mshikamano wa kijamii.

Pichani ni wananchi wa kata ya Machame Magharibi wilaya ya Hai wakipanda miti ( Picha na Vivian Kweka)

Aidha,Diwani Munisi  pamoja na wananchi wa kata ya Machame Magharibi wamemtakia maisha marefu na afya njema  Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na kwamba wanaungana na watanzania wengine katika siku hii muhimu kwa Rais Dkt Samia.

Hata hivyo Kata ya Machame Magharibi inaendelea kuwa mfano wa kuigwa katika uhifadhi wa mazingira na shughuli hii ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha kuwa mazingira yanahifadhiwa kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Sauti ya Diwani wa Kata ya Machame Magharibi Martin Munisi akizungumza wakati wa zoezi la upandaji miti