Boma Hai FM

Uroki Bomang’ombe watumia mapato ya ndani kuondoa adha ya maji

22 January 2026, 6:26 pm

Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Hai ( katikati) akiwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya Ndg. Wang’uba Maganda ( mwenye suti Nyeusi) na mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Mhe. Edmund Rutaraka ( kushoto mwenye nguo Nyekundu) pamoja na viongozi wengine wa wilaya ya Hai (Picha na Gasper Joseph)

Bodi ya Maji Uroki Bomang’ombe wametumia fedha za mapato yao ya ndani ili kutatua changamoto ya maji kwa wananchi wa wilaya ya Hai, mkuu wa wilaya ya Hai na Viongozi wengine wamepongeza juhudi hizo za kutatua adha ya maji kwa wananchi.

Na Gasper Joseph, Hai-Kilimanjaro

Mkuu wa wilaya ya Hai Hassan Bomboko ameipongeza bodi ya maji Uroki Bomangombe kwa jitihada zake za kupunguza kero ya maji kwa wananchi kwa kutumia fedha za mapato yake ya ndani.

Bomboko ameyasema hayo wakati wa kupokea mabomba ya kupanua mradi wa maji Uroki Boma ngo`mbe yenye thamani ya shilingi milioni 120 kwa ajili ya  ya mradi mpya wa chanzo cha mkomoshini unaolenga kuongeza maji takribani lita laki nane kwa siku.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Hai Mhe. Hassan Bomboko akizungumza wakati wakupokea mabomba yakupanua mradi wa maji wenye thamani ya sh. millioni 120

Nae mwenyekiti wa Halmashauri ya Hai ambae pia ni diwani wa kata ya Muungano Muh Edimundi Rutaraka ameishukuru bodi ya maji  Uroki Bomang`ombe Pamoja na RUWASA kuona umuhimu wa kutumia vyanzo vyake vya ndani na usimamizi mzuri wa rasilimali zilizopo kwa kuwekeza fedha nyingi kwenye mrdi huo utakao ongeza upatikanaji wa maji kwa wananchi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Hai Wang`uba  Maganda amesema kuwa ilani ya chama hicho imetendewa haiki na bodi ya maji Uroki Bomang`ombe kwani maji ni huduma muhimu kwa jamii na chama chake kinasimamia huduma ziwe bora kwa wananchi.

Pichani ni meneja wa bodi ya maji uroki Bomang’ombe Eng. Arnold Mbaruku wakati wa kupokea mabomba kwaajili yakupanua mradi wa maji (Picha na Gasper Joseph)

Akizungumza wakati akitambulisha mradi huo meneja wa maji bodi ya  maji Uroki Bomang`ombe mhandisi Arnold Mbaruku amesema kuwa bodi hiyo inatekeleza mradi huo kwa makusanyo yake ya ndani kwa zaidi ya shilingi milioni mia mbili hadi kukamilika kwake ili kuongeza na kuboresha huduma yam aji kwa wateja wake.

Sauti ya Meneja wa bodi ya maji uroki Bomang’ombe mhandisi Arnold Mbaruku akizungumza wakati wakupokea mabomba yakupanua mradi wa maji wenye thamani ya sh. millioni 120