Boma Hai FM

Vijana wapewa elimu ya matumizi bora ya mbegu za maharage ya lishe

28 May 2025, 10:07 pm

Baadhi ya vijana waliohudhuria katika mafunzo ya udhibiti ubora wa mbegu za maharage ya lishe ( Picha na Henry keto)

Mafunzo ya udhibiti ubora wa mbegu za kilimo yanayotolewa na taasisi ya (TOSCI) kwenye mradi wa Youth Enterprenuership for the future of food and agriculture (YEFA)

Na Henry keto, Hai-kilimanjaro

Kaimu mkurugenzi wilaya ya Hai ambaye pia ni Afisa Kilimo wilaya David Lekey amewaasa vijana kuchangamkia fursa kwenye Kilimo hasa cha umwagiliaji.

‎Lekey amewaasa vijana wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwaajili ya elimu ya Udhibiti ubora wa mbegu za maharage lishe, yaliyoandaliwa na shirika la Youth Entrepreneurship for the future of food and agriculture (YEFA).

Kaimu Mkurugenzi wilaya ya Hai David Lekey (Picha na Henry Keto)
Sauti ya Kaimu Mkurugenzi wilaya ya Hai David lekey akizungumza kuhusu Faida ya Mafunzo hayo kwa wilaya ya Hai

Afisa lishe mkoa wa Kilimanjaro Rehema Napegwa ameeleza umuhimu WA lishe hasa kwa akina mama na watoto, amesema mkoa wa Kilimanjaro una asilimia 20 sawa na watoto 48,000 wanahali ya udumavu jambo linalosababishwa na lishe duni.

‎Amewaasa jamii kuzingatia makundi yote sita ya vyakula ikiwemo jamii ya maharage lishe, ili kutenganisha kati ya nyama na maharage lazima tutumie vyakula mchanganyiko kwasababu maharage yana protein kama nyama lakn nyama ina mafuta mengi ganayosababisha uzito uliopitiliza

Sauti ya afisa lishe Mkoa wa Kilimanjaro Rehema Napegwa akitoa takwimu za udumavu unaotokana na ukosefu wa lishe kwenye mkoa wa Kilimanjaro

Afisa lishe wilaya ya Hai silvania kulaya amesema lishe ni muhimu hasa kwa wanawake wajawazito na wanaoenda kujifungua.
‎Amezungumza hayo wakati wa mafunzo ya Udhibiti ubora wa mbegu za maharage lishe anayotolewa na shirika la youth Entrepreneurship for the future of food and agriculture (YEFA) wakishirikiana na Taasisi ya kiserikali ya Tanzania Official seed certification institution (TOSCI)

Sauti ya Afisa Lishe Wilaya ya Hai Silvania Kulaya akizungumza Faida ya Maharage ya lishe katika mafunzo ya udhibi ubora wa mbegu

Nae Marium mwambati ambaye ndie manager mradi wa YEFA amesema mradi huu utakuwa na tija kwenye Kilimo kwasababu katika jamii yetu kimekuwa na shida ya mbegu Bora, kwahiyo elimu hii itasaidia vijana kuwa wakulima waziri katika uzalishaji wa maharage lishe ili kuzalisha na kuongeza kipato na kufanya Kilimo chenye tija.

Manager mradi wa YEFA Marium Mwambati (Picha na Henry keto)
Sauti ya Manager mradi Marium Mwambati akizungumza kuhusu mafunzo yanayotolewa kwa vijana

‎Nao vijana waliohudhuria mafunzo hayo wamesema mafunzo hayo yatawasaidia katika Kilimo chao ili kuongeza uzalishaji wa maharage

Sauti ya Vijana walionufaika na elimu ya udhibiti ubora wa mbegu za kilimo