Boma Hai FM

Milioni 300 zatolewa kwa vikundi 46 Siha

24 May 2025, 5:22 pm

Pichani ni viongozi mbalimbali wa halmashauri ya wilaya ya Siha pamoja na vikundi vilivyopata mkopo(picha na Bahati Chume)

” Kama mnavyofahamu wilaya hii ipo kwenye wilaya kumi za majaribio katika utoaji mikopo,niwajibu wetu kufanya vizuri ili na wengine wa wilaya zingine waweze kuiga “

Na Elizabeth Mafie -Siha Kilimanjaro.

Mkuu wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro Dkt Christopher Timbuka amevitaka vikundi vya wanawake,vijana na walemavu  vilivyopata mkopo  wa asilimia kumi ya halmashauri,kutumia mikopo hiyo kwa malengo walioainisha wakati walipokuwa wakiomba mikopo hiyo.

Kauli hiyo ameitoa Mei 23,2025   wakati  akikabidhi mfano wa hundi ya zaidi ya sh,300 milion  kwa vikundi 46  katika ukumbi wa halmshauri ya wilaya ya Siha.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mfano huo wa hundi ,amevitaka vikundi vilivyopata fedha hizo,kwenda kutumia fedha hizo kwa malengo makhususi.

” Kama mnavyofahamu  wilaya  hii ipo kwenye Wilaya za 10 za  majaribio katika utoaji mikopo,,niwajibu wetu kufanya vizuri ili na wengine wa wilaya zingine waweze kuiga “amesema Timbuka

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Siha Dkt Christopher Timbuka

Kwa upande wake Dancani Urasa Mwenyekiti wa halmshauri hiyo,amempongeza Mkurungenzi Mtendaji wa halmshauri hiyo Haji Mnasi kwa ukusanyaji mzuri wa mapato ya ndani na kwamba mikopo iliyotolewa kwa vikundi hivyo inatokana na makusanyo ya ndani ya halmashauri.

Nae mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo  Haji Mnasi amesema anamshukuru Rais Dkt Samia Suluhuu Hassani, kwa kurejesha utoaji wa mikopo ya asilimia kumi  kwa wananchi .

“Leo tumefanikiwa kutoa kiasi cha sh 300 milioni kwa vikundi hivyo vilivyotajwa baada ya wiki mbili zinatarajiwa kutolewa kwa vikundi vingine kiasi cha Zaidi ya shilingi milioni mia mia tatu .Amesema Mnasi”

Pichani ni Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Siha Haji Mnasi(aliyevaa tisheti nyeupe)akiwa na kikundi cha vijana kilichopata mkopo(picha na Bahati Chume)

Samwel Adu afisa mtendaji mkuu wa bank ya uchumi wilaya ya Siha amesema kwa kushirikiana na halmashauri,wametoa elimu ya fedha kwa wanufaika wa vikundi 46 katika awamu hiyo ya kwanza.

Sauti ya Samweli Adu Mtendaji mkuu Bank ya Uchumi wilaya ya Siha.

Kaale lukundo mmoja ya wanufaika wa mikopo hiyo, amesema wanaishukuru halmshauri kwa mikopo hiyo na kuahidi  kurejesha kwa wakati ili na vikundi vingine vinufaike.