Boma Hai FM
Boma Hai FM
20 May 2025, 10:10 am

Mapokezi ya mwenyekiti wa mtaa wa Kingereka aliyechaguliwa kwa tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) baada ya kuhama chama hicho na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Na Henry keto, Hai-Kilimanjaro
Mwenyekiti wa mtaa wa Kingereka A Dastan kimaro aliyechaguliwa kwa tiketi ya chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA leo amerudisha kadi ya chama hicho na kuhamia chama cha Mapinduzi CCM
Dastani ameshukuru chama cha mapinduzi kwa kukubali ombi lake la kuhamia kwenye chama hicho jambo liliopokelewa kwa furaha kubwa na viongozi na wanachama wa chama hicho na kuahidi kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa kwa maslahi ya wananchi wote, vilevile amewashukuru wananchi wa kingereka kuendelea kumuamini na kumchagua kuwa kiongozi wao
Mwenyekiti wa kata ya Bondeni exaudi Abinadabu Masawe amewaasa wenyeviti wote wa kata ya bondeni kujenga usawa kwa wananchi na safu ya uongozi kuanzia juu chini na kati ili wananchi waweze kuleta matatizo yao kwa viongozi wao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi tawi la kingereka ndg Hasheem sway amempongeza mwenyekiti Dastani na kumuahidi ushirikiano mkubwa katika utendaji kazi akiwa ni mwananchama na mwenyekiti wa kingereka kwa tiketi ya chama cha mapinduzi ccm.