Boma Hai FM

CRDB yakabidhi darasa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum

16 May 2025, 12:50 pm

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro(kulia) na Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi CRDB (kushoto) pamoja na viongozi wengine wa serikali na bank ya CRDB wakati wa uzinduzi wa darasa moja la watoto wenye mahitaji maalumu (Picha na Henry keto)

Crdb bank wilayani Hai mkoani Kilimanjaro yajenga darasa moja la wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule ya Msingi Uswaa lenye thamani ya Shilingi Millioni 25 ,hafla ya makabidhiano yafanyika.

Na Henry keto .Hai-Kilimanjaro

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Nurdin Babu amepokea darasa moja lenye thamani ya Shilingi Milioni 25 lililojengwa Kwa ufadhili wa Bank ya CRDB kwaajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule ya Msingi Uswaa wilayani Hai.

Katika uzinduzi huo ametoa wito kwa Wananchi kulitunza darasa hilo ambalo ni muhimu sana hasa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu, pia amewaomba Wananchi kuwa Karibu nao na kuwapa kipaumbele na upendo kama ilivyo kwa watoto wengine kwenye familia.

Aidha ameishukuru Bank ya CRDB kwa kujitolea kujenga darasa hilo na kuomba kuendelea kufanya hivyo kwasababu imekuwa ni desturi kwao kufanya hivyo, pia amewaomba Wananchi wa Kilimanjaro kujitoa kufanya maendeleo wasisuburi serikali ifanye, pale inapowezekana wao kufanya wafanye ili kuleta maendeleo katika Mkoa wa Kilimanjaro.

Vile vile ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa Fedha kwaajili yakuendeleza na kujenga miradi mingine mipya ambapo kwa kipindi cha miaka minne ameshatoa zaidi ya Trilioni 1.2 kwaajili ya kuleta maendeleo katika Mkoa wa Kilimanjaro.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu akihutubia wakati wa hafla ya kupokea darasa moja kutoka Bank ya CRDB

Mhe.Nurdin Babu ametoa wito kwa Wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro kujitokeza kuboresha taarifa zao katika daftari la kupiga kura kwa awamu ya pili linaloanza May 16,2025.

Amewatoa hofu Wananchi kuhusu zoezi la upigaji kura utakuwa wa amani na utulivu hakuna lolote baya litajitokeza, Serikali ya Mkoa kwakushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa imejipanga vizuri kulinda amani wakati wote wa uchaguzi, hivyo Wananchi wajitokeze kupiga kura.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu akizungumza kuhusu uboreshaji wa daftari la mpiga kura na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025
Darasa liliojengwa kwa udhamini wa bank ya CRDB kwaajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule ya msingi Uswaa lenye thamani ya shillingi milioni 25 (Picha na Henry keto)

Nae Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Bank ya CRDB ameishukuru serikali kwa kuendelea kuleta maendeleo kwa Wananchi wake,na bank inaunga mkono juhudi za kuleta maendeleo kwa Wananchi wote, vile vile ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya hai kwa kuusimamia mradi wakati wa ujenzi hadi kukamilika kwa viwango vinavyohitajika mpaka kufikia kukabidhi darasa kwaajili ya matumizi.

Katika hotuba yake amesema bank ya CRDB watakarabati Madarasa mawili ya shule hiyo kwaajili yakuunga mkono juhudi za Serikali na ikiwa ni miongoni mwa sera zao ambazo ni Afya, Elimu na Mazingira, na wanaendelea kutekeleza.

Sauti ya Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa bank ya CRDB wakati wakukabidhi darasa moja lenye thamani ya shillingi millioni 25 kwaajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule ya msingi Uswaa