Highlands FM
Highlands FM
6 June 2025, 4:29 pm

Makanisa sita ya Ufufuo na Uzima yafungwa Mbeya kufuatia agizo la serikali
Na Samwel Mpogole
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limefunga makanisa sita ya huduma ya Ufufuo na Uzima yaliyokuwa yakiendelea na shughuli zake kinyume na tamko la serikali lililotolewa Juni 2, 2025 kupitia Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, SACP Benjamin Kuzaga, amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la serikali linalozuia huduma zote za makanisa ya Ufufuo na Uzima kote nchini huku akisema makanisa yaliyofungwa ni yaliyopo ZZK Mbalizi, Mtaa wa Mnadani Rujewa (Wilaya ya Mbarali), pamoja na wilaya za Chunya, Rungwe, Kyela, na Jiji la Mbeya.
Kuzaga amesema kuwa Katika tukio jingine, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na maafisa kutoka Kampuni ya Mawasiliano ya Halotel linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za wizi na usafirishaji wa vyuma vya minara ya mawasiliano ya kampuni hiyo.
Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi kushirikiana katika kufichua vitendo vya uhalifu vinavyoathiri maendeleo ya sekta ya mawasiliano na usalama wa nchi kwa ujumla.