Boma Hai FM

Madereva wakumbushwa kukagua magari kuepusha ajali

13 March 2026, 2:45 pm

Pichani ni Sajenti Ramadhani Juma kutoka kituo cha polisi Bomang’ombe kitengo cha usalama barabarani akiwa katika studio za radio Boma Hai Fm(picha na Elizabeth Mafie)

Kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali hapa nchini wito umetolewa kwa watumiaji wa barabara pamoja na madereva kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa vyombo vyao vya moto ili kuepusha ajali.

Na Oliva Joel

Hai -Kilimanjaro

Katika kipindi hiki cha mvua, madereva na watumiaji wengine wa barabara wametakiwa kukagua vyombo vyao vya moto mara kwa mara ili kuepuka ajali.

Hayo yameelezwa leo Machi 13, 2026 na Sajenti  Ramadhani Juma  kutoka kituo cha Polisi Bomang’ombe, kitengo cha usalama barabarani, alipokuwa akizungumza katika kipindi cha siku mpya  kinachorushwa na  Radio Boma Hai FM.

Amesema kuwa ukaguzi wa vyombo vya moto mara kwa mara humwezesha dereva kutumia chombo chake kwa kujiamini na kusaidia kuepusha madhara kwa watumiaji wengine wa barabara.

Aidha, ameongeza kuwa ukaguzi wa chombo cha moto unapaswa kufanyika mara kwa mara bila kujali kama dereva atasafiri umbali mrefu au mfupi, ili kuhakikisha usalama wake na wa watumiaji wengine wa barabara.

Sauti ya Sajenti Ramaddhani Juma kutoka kituo cha polisi Bomang’ombe kitengo cha usalama barabarani.

Sajenti Ramadhani amewapongeza madereva wengi ambao wamekuwa wakikagua vyombo vyao mara kwa mara na kwamba ajali nyingi zinazotokea barabarani si zote zinatokana na ubovu wa magari, bali baadhi husababishwa na madereva kutokuzingatia sheria za usalama barabarani pamoja na kutokuwa makini wanapokuwa wanaendesha.