Boma Hai FM

Sheikh Mlewa aongoza waislam Kilimanjaro sikukuu ya Eid-el-Fitir, ataka amani

31 March 2025, 1:44 pm

Sheikh wa mkoa wa Kilimanjaro Shaban Mlewa(picha na Bahati Chume)

Ikiwa ni sikukuu ya Eid-el-Fitir kote duniani, ambapo waumini wa dini hiyo mkoa wa Kilimanjaro wilaya ya Hai watakiwa kuendelea kuishi maisha ya kumpendeza mwenyenzi Mungu na kuendelea kulinda amani.

Na Elizabeth Mafie

Waumini wa Dini ya kiislamu mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuendelea kudumisha amani katika kuelekea uchanguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba mwaka huu.

Hayo yamesemwa Machi 31 2025 na Sheikh wa mkoani Shaabani Mlewa wakati wa Maadhimisho ya sikukuu ya Eid-el-Fitir iliyofanyika Msikiti wa Shafii Bomango’mbe wilayani Hai mkoani hapa.

Akizungumza na waumini hao mara baada ya swala hiyo ya Eid ,amewataka Waislamu kuendelea kudumisha amani na upendo kwani ndiyo msingi mzuri wa maisha.

“Ni kweli uchanguzi mkuu unakuja,na kila uchanguzi unapokuja uinakuja na vitimbwi vingi , sasa akili kichwani,wewe mwenyewe kama muislamu inatakiwa kuwa wa kwanza kutunza amani”amesema Mlewa

Aidha katika uchanguzi ujao amewataka Wananchi kuchagua viongozi wazuri , ambao watawaongoza na wanaoamini lakini pia waumini hao wajitokeze na kugombea nafasi mbalimbali.

Sauti ya Sheikh wa Mkoa wa Kilimanjaro Shaban Mlewa.

“nyinyi wenyewe ingieni Tupate watu tutakao waamini,watakao tusaidia ,tunaitaji maendeleao,ukienda Kwa Mwenyekiti wa kijijii kusiwe na ukirutumba ,nataka kumuonea Mbunge anakata simu hapana,tunataka Viongozi wazuri wasema ukweli”. Amesema Shekhe Mlewa.

Waumini wakisikiliza mawaidha katika msikiti wa kwa Shafii Bomang’ombe(picha na Bahati Chume)

Awali Imamu wa Msikiti huo, Athumani Hamis,amesema  kuwa anamshukuru Mungu kwakuhitimisha vyema mwezi mtukufu wa Ramadhani na kwamba waumini wa dini hiyo wanapaswa kuyaishi yale waliyoelekezwa katika kipindi chote cha mfungo.

 Hivyo kuwakumbusha waumini kuendelee kufanya mema kama walivyokuwa wakifanya  wakati wa mfungo wa Ramadhan,kwani kurudi kufanya maovu ni jambo baya  mbele ya Mwenyezi Mungu  na unahesabika  kuwa umepata hasara.