Highlands FM

Mwalunenge awakumbusha watia nia wajibu wao kwa wananchi

1 July 2025, 12:51

Patrick Mwalunenge .Picha na Mwandishi wetu

Baadhi ya wabunge katika maeneo mbalimbali nchini wakirejesha fomu ambapo zoezi hilo linatarajiwa kufungwa kwesho julai 2,2025.

Na Lameck Charles

Mtia nia wa ubunge wa Jimbo la Mbeya mjini (CCM) Patrick Mwalunenge amewakumbusha watia nia wenzake kuachana na uchonganishi ili kuepusha mpasuko ndani ya Chama, badala yake wawaeleze wananchi nini watafanya ikiwa watateuliwa.

Mwalunenge ametoa tahadhari hiyo  wakati akirejesha fomu ya kuwania Nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbeya mjini fomu hiyo aliyochukuliwa na Makundi ya Wafanyabaishara na Usafirishaji.

Sauti Mwalunenge

Aidha ametoa wito kwa wananchi mkoa wa mbeya kujitokeza kwa wingi na kutia nia ya kuwatumikia wananchi ikiwa bado zoezi  la uchukuaji fomu bado halijafungwa.

Sauti Mwalunenge 2

Katika hatua nyingine Mwalunenge amewashukuru wananchi wa Mbeya kwa mapenzi ya dhati waliyomuonesha huku akiahidi endapo atapata nafasi ya kuwaongoza hatowangusha

Sauti Mwalunenge 3

kwa Mujibu wa ratiba ya Chama Cha Mapinduzi mwisho wa kuchukua  na kurejesha fomu kwa ajili ya kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya ubunge na udiwani ni Julai 2,2025 saa kumi jioni.