Highlands FM

PCT yawanoa mawakala kuelekea msimu mpya wa mavuno 

7 June 2024, 17:03

Afisa pareto mkoa wa mbeya na songwe Mussa Malubalo akitoa elimu kwa mawakala na wakulima wa zao la pareto Mbeya na Songwe

Na Lameck Charles

Highlands Fm Radio

Kampuni ya Pareto Tanzania (PCT) imewapa mafunzo mawakala wa kampuni hiyo ikiwa ni maandalizi kabla ya kuanza Rasmi Kwa mavuno 

Mafunzo hayo yaliyofanyika eneo la Ilembo umalila yamewakutanisha mawakala,wakulima waweze kupata elimu ni maua gani ambayo ni bora kwa kuvuna ili kuweka ubora wa zao hilo.

Kwa Upande wake Gerad Joseph ambye ni afisa kutoka kampuni ya pareto Tanzania (PCT) amesema kwa msimu kwa 2022/23 kamapuni hiyo ilipata hasara ya zaidi ya shilingi billion1 huku akiishukuru serikali ya mkoa wa mbeya kwa kuweka utaratibu kwa kila kampuni ya ununuzi wa pareto  kutonunua maua yasiyo bora.

Sauti Gerad

Mussa Malubalo ni Afisa Pareto Mkoa wa Mbeya na Songwe amesema wao kama PCT wamekuwa wakiwapa mafunzo wakulima Kabla ya kuanza Kwa Msimu Ili kuepuka kupata maua yasiyo Bora kama ilivyotokea  kwa mwaka jana.

Sauti Mussa
Baadhi ya Mawakala na wakulima wakipatiwa mafunzo juu ya zao la Pareto
Sauti Mawakala

Kampuni ya Pareto Tanzania (PCT) imewakutanisha mawakala wake na wakulima Toka mikoa ya Mbeya na Songwe ikiwa ni Utekelezaji wa Makubaliano yaliyotolewa hivi Karibuni na Serikali ya Mkoa wa Mbeya.