Highlands FM

Wanahabari Mbeya wakumbushwa kujiandaa maisha ya uzeeni

11 June 2025, 16:33

Meneja wa PSSSF Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Ramadhani Mgaya. Picha na Samwel Mpogole

Waandishi wa habari Mbeya waaswa kujiandaa kwa maisha baada ya utumishi

Na Samwel Mpogole

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari mkoani Mbeya wamepewa mafunzo na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), yenye lengo la kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii pamoja na kuwa mabalozi wa kuelimisha umma juu ya maandalizi ya maisha ya kustaafu.

Mafunzo hayo yamefanyika jijini Mbeya katika ukumbi wa Mgwasi, yakihusisha majadiliano ya kina kati ya wataalamu wa PSSSF na wanahabari kuhusu umuhimu wa kuwa na maandalizi bora ya baada ya utumishi ambapo  Meneja wa PSSSF Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Ramadhani Mgaya na Afisa Mahusiano kutoka Makao Makuu ya PSSSF Dodoma, Rehema Mkamba Wameeleza nafasi ya waandishi wa habari katika kufikisha elimu ya hifadhi ya jamii kwa umma

Sauti ya Rehema Mkamba

Kwa upande wake, mmoja wa wanachama wa PSSSF ambaye pia ni mstaafu, Vicent Msola, ameshuhudia kwa namna mafao yake yalivyopatikana kwa haraka baada ya kustaafu, jambo linaloonesha ufanisi wa mfumo huo.

Sauti ya Vicent Msola

Naye Mweka Hazina wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mbeya (Mbeya Press Club), Bi. Rukia Chasanika, amesema mafunzo hayo yamekuwa na tija kwa wanahabari, hasa kwa kuwaongezea uelewa juu ya haki na wajibu wao katika hifadhi ya jamii.

Sauti ya Rukia Chasanika

Mafunzo hayo ni sehemu ya mikakati ya PSSSF kuhakikisha elimu ya hifadhi ya jamii inawafikia wadau mbalimbali, wakiwemo wanahabari ambao wana mchango mkubwa katika kuibadilisha jamii kupitia taarifa.