Highlands FM

TAKUKURU yahimiza waandishi kupambana na Rushwa wakati wa uchaguzi

4 June 2025, 18:57

Mkuu wa TAKUKURU Mbeya Maghela Ndimbo. Picha na Samwel Mpogole

Waandishi wa habari wamehimizwa kushiriki katika mapambano dhidi ya Rushwa hasa Taifa linapoelekea katika uchaguzi mkuu

Na Samwel Mpogole

Taaisisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa mbeya imewataka waandishi wa habari kushirikiana nao bega kwa bega, hasa katika kipindi hiki Taifa linapoelekea katika Uchaguzi Mkuu.

Hayo yamesemwa na Maghela Ndimbo, Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya, alipokuwa akizungumza na Highlands Fm. Ndimbo amesema ushiriki wa waandishi wa habari ni muhimu sana katika mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa, kwani vyombo vya habari vina mchango mkubwa katika kuelimisha umma na kufichua maovu.

Sauti ya Maghela Ndimbo

Kwa upande wake, Felix Mwakyembe, mwanahabari mkongwe, ametoa wito kwa waandishi wa habari kuwa makini dhidi ya matumizi ya akili mnemba, kwani kutoitumia kwa umakini inaweza kuharibu mchakato wa uchaguzi na hata kuwaingiza matatizoni.

Sauti ya Felix Mwakyembe

Katika hatua nyingine, Ndimbo amewataka wananchi kwa ujumla kushirikiana na mamlaka hiyo kwa kutoa taarifa mapema pindi wanapohisi au kushuhudia viashiria vya rushwa.

Sauti ya Maghela Ndimbo

TAKUKURU inaendelea na juhudi zake za kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya rushwa na umuhimu wa kushiriki katika uchaguzi kwa njia ya haki na uwazi, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuhakikisha uchaguzi mkuu ujao unakuwa huru na wa haki