Mufindi FM

TAEEs yatoa mafunzo kwa bodi za maji 15 Mufindi

21 September 2023, 18:46

Na Kelvin Mickdady -MufindiFM

Bodi za kusimamia vyanzo na usafi wa maji wilayani Mufindi zimetakiwa kuboresha mfumo wa ufanyaji kazi ili kuongeza mapato ya serikali kupitia bodi hizo.
Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa halmshauri ya wilaya ya Mufindi Mhe. Festo Mgina wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo vyombo vya watoa huduma ya maji na kusema kuwa inatakiwa kuwe na ushirikiano kati ya viongozi wa bodi na jamii.

Sauti ya Festo Mgina

Sanjari na hayo Mhamasishaji mradi wa shirika la wahandisi Mazingira Tanzania Bi. Sayun Mbiga amesema kuwa mafunzo hayo yanakwenda kuongeza ufanisi katika utendaji kazi kwenye bodi za maji.

Sauti ya Bi. Sayun Mbiga

Kwa upande wake Afisa maendeleo Kutoka Wakala wa Maji na Usalama wa Mazingira Vijijini RUWASA Josephat Kyando ameitaka jamii kulipia maji ili kuongeza mapato.

Sauti ya Mhandisi Kyando

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamesema kuwa elimu hiyo waliyoipata inakwenda kubadili mfumo wao wa utendaji kazi.

Sauti ya Washiriki

Mafunzo ya kuwajengea uwezo vyombo vya watoa huduma ya maji Ngazi ya jamii (CBWS) Yamefunguliwa Sept 20 Na kutamatika leo Septemba 21/09 Kwa halmashauri ya wilaya ya Mufindi.