Uyui FM Radio

ACP Deleli: Waathirika zaidi wa ajali ni bodaboda

12 July 2024, 5:45 pm

Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya sheria za usalama barabarani.Picha na Zaituni Juma

Chuo cha mafunzo ya udereva Utalii East Afrika – Tabora kimeratibu mafunzo bure kwa waendesha Bodaboda,bajaji na maguta zaidi ya 500 Manispaa ya Tabora  kwa kipindi cha mwezi 1 kwa lengo la   uzingatiaji  wa sheria za usalama barabarani.

Na Zaituni Juma

Waendesha pikipipiki za abiria maarufu kama Bodaboda wametajwa kuwa, ndio waathirika zaidi wa ajali za barabarani nchini ukilinganisha na watumiaji wengine wa barabara.

Mkuu wa dawati la elimu ya usalama na mafunzo barabarani Tanzania ACP Michael Deleli amesema hayo wakati akizungumza kwenye hafla ya kufunga mafunzo ya watumiaji wa vyombo vya moto yaliyofanyika eneo la machinga Complex Manispaa ya Tabora.

ACP Deleli akizungumza na wahitimu pamoja na wananchi.Picha na Zaituni Juma
Sauti ya ACP Deleli

Kwa upande wake mkurugenzi wa chuo cha Utalii cha East Afrika Tabora Shabani Mrutu amesema mafunzo hayo yatasaidia kupunguza ajali za barabarani ambazo zinaleta  athari kubwa kwa vijana na jamii kwa ujumla.

Mkurugenzi chuo cha Utalii East Afrika-Tabora Shabani Mrutu wakati akizungumza.Picha na Zaituni
Sauti ya Shabani Mrutu

Baadhi ya wahitimu wa mafunzo hayo Elizaberth Bimla na Isaya Ibrahimu  wamesema wamepata uelewa wa kutosha juu ya matumizi sahihi ya  alama za barabarani tofauti na hapo awali.