Uyui FM Radio

Dkt. Biteko: Tangulizeni maslahi ya watanzania masikini

7 July 2024, 7:18 pm

Baadhi ya viongozi wa ushirika. Picha na Mohamed Habibu

Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani kitaifa yamefanyika mara ya nne mfululizo mkoani Tabora yakibeba kaulimbiu isemayo “Ushirika hujenga kesho iliyo bora”

Na Nicholaus Mwaibale

Naibu Waziri Mkuu na waziri wa nishati Daktari Dotto Biteko amewataka viongozi wa ushirika nchini kufanya kazi kwa kutanguliza maslahi ya watanzania masikini ili kuwaisaidia kukuza uchumi.

Daktari Biteko ametoa maagizo hayo wakati wa kufunga maadhimisho ya siku ya Ushirika Duniani kitaifa ambayo yamefanyika katika viwanja vya nanenane Ipuli ,Manispaa ya Tabora.

Daktari Biteko akizungumza na wananchi.Picha na Mohamed Habibu
Sauti ya Daktari Biteko

Naye Waziri wa kilimo Hussein Bashe amesema  msimu huu Sekta ya Tumbaku imezalisha wastani wa tani laki moja ukilinganisha na mwaka jana ambapo zilizalishwa tani elfu 60 tu, huku akibainisha changamoto walizokumbana nazo wakulima katika kipindi hiki cha uzalishaji wa tumbaku.

Waziri wa kilimo Hussein Bashe akizungumza na wanashirika.Picha na Mohamed Habibu
Sauti ya waziri kilimo Bashe

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha amesema kuwa masoko ya tumbaku na pamba yanaendelea vizuri na wananchi wanaendelea na masoko bila manunguniko.

Rc Chacha akizungumza kabla ya mgeni rasmi.Picha na Mohamed Habibu