Uyui FM Radio

Wananchi milioni 1.6 wapatiwa chanjo ya UVICO 19 Tabora.

5 May 2024, 3:34 pm

Timu za usimamizi huduma ya afya wilaya ya Kaliua na Uyui.Picha na Zaituni Juma

Na Zaituni Juma

Serikali mkoani Tabora imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la CARITAS Tabora katika utoaji wa chanjo ya UVICO 19 ili kumfikia kila mwananchi.Na

Zaidi ya  watu milioni 1,600,000 wamepatiwa  chanjo ya UVICO 19 kwa mkoa wa Tabora tangu kuanza kutolewa  katika maeneo mbalimbali ikiwa ni sawa na asilimia  112.

Mganga mkuu wa mkoa wa Tabora Daktari Honorata  Rutatinisibwa amesema  hayo katika ukumbi wa JM Hoteli  wakati wa kuhitimisha mradi wa utoaji wa chanjo ya UVICO 19 kwa kipindi cha mwaka 2023 ulioratibiwa na shirika la Cartas Tabora.

Sauti ya mganga mkuu

Naye mkurugenzi wa shirika la CARTAS TABORA Padri Paschal Kitambi amesema wataendelea kutekeleza miradi mbalimbali ili kuigusa jamii moja kwa moja.

Padri Kitambi akizungumza na timu za Usimamizi wa afya.Picha na Zaituni Juma
Sauti ya Padri Kitambi

Kwa upande wake, Daktari wa shirika hilo MARIAMU MIKINDA amesema katika kutekeleza mradi wa utoaji wa chanjo ya UVICO 19 kwa kipindi cha mwaka mmoja wamefikia vituo vya afya 65 na kutoa chanjo kwa watu elfu 43 kwa wilaya za Kaliua na Uyui.

Daktari Mariam Mikinda.Picha na Zaituni Juma
Sauti ya Daktari Mariam