Uyui FM Radio

Dkt. Msonde: Walimu wekeni msingi mzuri wa lugha ya kiingereza

30 June 2024, 9:10 pm

Baadhi ya walimu wakimsikiliza Dkt. Charles Msonde. Picha na Elisha Lusatila

Dkt. Charles Msonde amekuwa na ziara katika mikoa mbalimbali ikiwemo Kagera na Tabora ambapo pamoja na mambo mengine ametumia fursa hiyo kuzungumza na walimu.

Na Elisha Lusatila

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI (Elimu) Dkt. Charles Msonde amewataka walimu mkoani Tabora kuweka msingi mzuri kwa wanafunzi katika ufundishaji wa lugha ya kingereza ili wasipate changamoto wakifka elimu ya sekondari.

Dkt. Msonde amesema hayo wakati akizungumza na walimu, walimu wakuu, wakuu wa shule, maafisa elimu wa kata na wilaya pamoja na wasimamizi wa elimu katika wilaya ya Uyui kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Idete iliyopo wilayani humo.

Dkt. Msonde akizungumza na walimu.Picha na Elisha Lusatila

Awali  Mkuu wa Wilaya ya Uyui  Zakaria Mwansasu ameiomba serikali kuongeza nguvu kwenye vituo shikizi vilivyopo wilayani Uyui ili kuepuka  utoro kwa wanafunzi  kutokana  na kutembea umbali mrefu.

Mkuu wa Wilaya Mwansasu akizungumza na Dkt. Msonde ofisini kwake. Picha na Elisha Lusatila