Uyui FM Radio

Bomoabomoa yawafikia waliovamia hifadhi ya barabara Tabora

28 May 2024, 5:39 pm

maduka yaliyo ndani ya hifadhi ya barabara ya Ushokola hadi Kasungu.Picha na Mohamed Habibu

Kwa mujibu wa sheria ya ardhi kifungu namba 6 na sheria ya barabara namba 13 ya mwaka 2007 na kanuni ya mwaka 2009 kifungu cha 29 kwa pamoja vinaeleza umuhimu wa kutunza na kuheshimu hifadhi hizo.  

Na Zaituni Juma

Wakala ya Barabara Nchini  TANROADS mkoa wa Tabora imetoa siku 30 kwa wananchi waliovamia  kujenga nyumba na vibanda kwenye barabara ya Ushokola kaliua mjini hadi Kasungu  kuhakikisha wanabomoa kwa hiari yao wenyewe.

Akizungumza na wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo,Msimamizi wa TANROADS mkoa wa Tabora Mhandisi Enock Mitenda amesema baada ya muda huo kumalizika hatua zitachukuliwa kwa watakao kiuka.

Msimamizi wa TANROADS mkoa wa Tabora Mhandisi Enock Mitenda akizungumza na wananchi
Sauti ya mhandisi Mitenda

Kwa upande wake diwani wa kata ya Kaliua NESTORY ELIAS amekiri kuwa uvamizi huo wa hifadhi ya barabara ni kosa hivyo watasimamia utekelezaji wa suala hilo pasipo kuathiri mwananchi yoyote.

Diwani wa kata ya Kaliua NESTORY ELIAS akizungumza na wananchi
Sauti ya diwani NESTORY