Uyui FM Radio

Hospitali wilaya ya Tabora yapata vifaa tiba

14 August 2024, 9:56 am

Baadhi ya vifaa viliyokabidhiwa.Picha na Job Chimwaga

Vifaa tiba vilivyotolewa vina thamani ya zaidi ya shilingi milioni sita.

Na Salma Abdul

Mkuu wa mkoa wa Tabora Paul Chacha amepokea vifaa tiba ikiwemo viti mwenda pamoja na vitanda kwaajili ya kusaidia utoaji wa huduma mbalimbali za matibabu katika hospitali ya wilaya ya Tabora.

Akipokea msaada huo kutoka benki ya NMB tawi la Mihayo Tabora mkuu wa mkoa wa Tabora ameshukuru na kuahidi kuwa vitatunzwa vizuri.

Mkuu wa mkoa Chacha akikabidhiwa kiti mwendo na meneja NMB kanda ya magharibi.Picha na Chimwaga
Sauti ya mkuu wa mkoa

Meneja wa benki ya NMB kanda ya magharibi Restus Assenga amesema wametoa vifaa hivyo baada ya kupokea maombi kutoka katika hospitali hiyo.

Mkuu wa mkoa akipokea vitanda vya kulalia wagonjwa. Picha na Job Chimwaga
Sauti ya Assenga

Agness  Mathias  ni mmoja wa wananchi walioshuhudia upokeaji wa vifaa hivyo ambaye ni miongoni mwa wanaopata huduma katika hospitali hiyo amesema.

Sauti ya Agnes

Naye Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Daktari Gwamaka Edward ametoa shukrani kwa kupatikana kwa vifaa hivyo.

Sauti ya daktari Gwamaka