Uyui FM Radio

Afisa maendeleo-Msiwatelekeze  watoto kwa bibi na babu zao  

12 June 2024, 11:58 am

Badhi ya wanafunzi shule ya msingi Town school wakiwa kwenye muda wa mapumziko .Picha na Zaituni Juma

Kila ifikapo juni 12 ya kila mwaka  dunia inaadhimisha siku ya kupinga utumikishwaji wa Mtoto ambapo kwa mwaka huu imebeba kaulimbiua isemayo ‘’komesha utumikishwaji wa mtoto’’

Na Zaituni Juma

Wazazi na walezi wilayani Tabora wameaswa kutowatelekeza watoto wao kwa wazee suala linalochangia kwa kiasi kikubwa  utumikishwaji  kwenye maeneo mbalimbali.

Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Tabora Helena Mathias amseema hayo wakati akizungumza na UFR ikiwa ni maadhimisho ya siku ya  kupinga utumikishwaji wa mtoto duniani ambayo kimkoa yanafanyika kijiji cha Kalemela ‘B’ wilayani Urambo.

Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Tabora Helena Mathias akizungumza Studio.Picha na Zaituni Juma
Sauti ya Afisa maendeleo

Kwa upande wake Afisa mradi wa Taasisi ya Elimu bora Foundaution mwalimu Grace Kasoga amesema wamekuwa wakitoa elimu kwa walimu mashuleni ili kuzingatia utoaji wa adhabu kwa wanafunzi.

Mwalimu Grace Kasoga
Sauti ya mwalimu Grace Kasoga

Nae mhamasishaji wa shirika lisilo la kiserikali lilipo mkoani Tabora –CODEWA Happy Kitanga ameeleza mojawapo ya sababu za utumikishwaji wa watoto.

Happy Kitanga