Radio Jamii Kilosa

Elimu ya lishe yazidi kutoa matokeo chanya kata ya Berega

25 May 2025, 4:05 pm

Afisa lishe Elisha Kingu akigawa uji kwa watoto katika siku ya afya na lishe kijiji ilifanyika kijiji cha Berega. Picha na Asha Madohola

Serikali inaendelea kuwekeza katika elimu ya lishe, na kuongeza upatikanaji wa vyakula vyenye virutubisho muhimu kwa mama na mtoto na lengo ni kuhakikisha jamii inapata lishe bora na afya njema kwa maendeleo endelevu ya taifa.

Na Asha Madohola

Kata ya Berega wilayani Kilosa 24 Mei imefanya Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji kwa kushirikisha vijiji vyake vinne, ambapo wananchi walijifunza kwa vitendo namna ya kuandaa uji wa lishe bora ambapo watoa huduma za afya ngazi ya jamii (CHW) waliandaa uji huo na kutoa elimu juu ya umuhimu wa makundi sita ya chakula katika maandalizi ya lishe kwa watoto.

Sauti ya Mhudumu afya ngazi ya Jamii Bi Perisi Mhina
Afisa Mtendaji kata ya Berega Marry Fungo

Afisa Mtendaji wa Kata ya Berega Marry Fungo alisema siku ya afya na lishe kijiji imefanyika katika vijiji vinne umuhimu wa kuendelea kushirikiana na wataalamu wa afya na viongozi wa kijiji katika kuhakikisha elimu ya lishe inawafikia wananchi wote.

Sauti ya Mtendaji kata ya Berega Bi Marry Fungo
Afisa lishe wilayani Kilosa Elisha Kingu akipata uji kwenye siku ya afya na lishe kijiji cha Berega

Aidha Afisa Lishe wa Wilaya alitembelea baadhi ya vijiji na kutoa elimu ya kina kuhusu lishe bora kwa watoto chini ya miaka mitano, wajawazito na akina mama wanaonyonyesha huku akisisitiza kuwa ulaji wa makundi sita ya chakula ni muhimu ili kupata virutubisho vya kutosha ili kujenga afya imara kwa mama na mtoto, na kuzuia matatizo ya udumavu, ukondefu na uzito pungufu.

Sauti ya Afisa lishe wilaya Kilosa Ndg Elisha Kingu
Kaimu Mganga Mkuu Prosper Mlonge akigawa uji kwa watoto

Kaimu Mganga Mkuu Prosper Mlonge naye alihimiza elimu hiyo iendelee kutolewa kwa wananchi kwa kutumia mikutano ya kijiji, ili ujumbe uwafikie wengi kwa wakati mmoja. Amesema ushirikiano kati ya wataalamu wa afya na viongozi wa kijiji ni muhimu katika kufanikisha afua za lishe.

Sauti ya Kaimu Mganga Mkuu Prosper Mlonge
Bi Magreth Mkazi wa kijiji cha Mgugu

Wananchi waliopata elimu hiyo akiwemo Bi Magreth Maranda walionesha kufurahishwa na maarifa mapya waliyojifunza, huku wakiahidi kuyatumia katika familia zao kwa lengo la kuboresha afya za watoto na kina mama katika jamii yao.

Sauti ya Bi Magreth Maranda Mkazi wa Mgugu
Afisa lishe akigawa uji kwa watoto