Huheso FM

Wananchi wapongeza ulinzi shirikishi kutekeleza majukumu yake

July 30, 2024, 3:04 pm

Wakazi wa Kata ya Nyihogo iliyopo Manispaa ya Kahama Mkoani Shinyanga wameonyesha kufurahishwa na utendaji kazi wa Ulinzi shirikishi ambapo kwa asilimia kubwa umeweza kukabiliana na wimbi la vibaka na kuimalisha ulinzi na usalama.

Wakizungumza hii leo  wameeleza kuwa ,Ulinzi uliopo umesaidia kwani Vibaka wamepunguza kasi ya matukio ya ajabu na mpaka sasa raia wana amani hata wanapotembea usiku .

Pia wameongeza  kuwa Serikali za mitaa zizingatie umri inapopanga vikosi vya ulinzi na  kutoa mafunzo kwa Walinzi hao ili kuepuka migogoro inayotokea na Wananchi

Sauti ya wananchi wakizungumzia hali ya ulinzi na usalama ambapo wametoa pongezi zao kwa ulinzi kuwa imara

Kwa upande wao  Wajumbe wamesema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha kata hiyo  ya Nyihogo inaondokana na Matukio ya kiharifu yakiwemo ya upolaji,ukabaji na ubakaji,na wamesisitiza vijana wafanye kazi halali .

Sauti ya viongozi ya Mtaa wa Nyihogo wakizungumzia ulinzi shirikishi katika eneo lao

Mwenyekiti Idd Mitimingi ameongeza kwa Kusema kwamba atahakikisha vikosi vya ulinzi vinafanya kazi inavyositahili kwa kuzingatia maadili ya kazi yao na amewaomba Wananchi kutunza mali zao vizuri.