FM Manyara

NMB yatoa mil. 38.5 kusaidia vifaa shule, zahanati wilayani Babati

5 February 2026, 1:36 pm

Picha ya meneja wa kanda wa NMB Baraka Ladislaus akizungumza pembeni ya mkuu wa Wilaya ya Babati Emanuela Kaganda .

Na George Augustino

Benki ya NMB imetoa msaada wa madawati, mbao pamoja na mabati yenye jumla ya thamani ya shilingi million 38 na laki tano kwa shule ya msingi kiongozi, shule ya msingi soraa, shule ya msingi singu B, pamoja na zahanati ya imbilili,zilizopo wilayani babati mkoani manyara.

Akikabidhi vifaa hivyo mbele ya mkuu wa wilaya wa babati ambaye ndiye mgeni rasmi wa shughuli hiyo Emanuela Kaganda Meneja wa NMB  kanda ya kaskazini  Baraka Ladislaus amesema Benki ya nmb inatambua juhudi zinazofanywa na serikali  na benki hiyo inaunga mkono juhudi hizo katika kuboresha huduma za maendeleo ya jamii ikiwemo elimu na afya kwa kutoa sehemu ya faida inayoipata.

Sauti ya meneja wa kanda wa benki ya NMB

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Babati Emanuela Kaganda ameishukuru Benki ya NMB kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali katika kuhudumia jamii kwa kutoa misaada mbalimbali pamoja na huduma za kifadha wanazozitoa kwa uaminifu kwa watumishi wa umma na jamii kwa ujumla.

Aidha Dc Kaganda Alisisitiza utunzaji wa vifaa hivyo hasa madawati hayo ili viendelee kuzisaidia shule hizo pamoja na kuahidi ushirikiano kati ya serikali na Bank ya NMB BABATI mkoani Manyara.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Babati

Naye Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kiongozi mwalimu Omary Tindi ameishukuru Benki ya NMB kwa kuwasaidia madawati 50 ambayo yamesaidia kupunguza uhaba wa madawati katika shule hiyo na kuahidi kuendelea kuyatunza madawati hayo ili yaendelee kuwanafaisha wanafunzi wa shule hiyo.

Sauti ya mwalimu mkuu wa shule ya msingi kiongozi
Picha ya wanafunzi wa shule ya msingi Kiongozi wakiupongeza uongozi wa benki ya NMB kwakuwapa msaada wa madawati