Uvinza FM
Uvinza FM
30 July 2026, 6:28 pm

kuongeza juhudi na kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati uliopangwa
Na. Abdunuru Shafii
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Kanali Michael Ngayalina, amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja linalovuka Mto Luiche, unaotenganisha Kijiji cha Kinazi na Kijiji cha Nyamihanga kilichopo Kata ya Janda. Daraja hilo ni kiungo muhimu kinachounganisha Kata za Kinazi na Munzeze na linatarajiwa kuboresha mawasiliano na usafiri katika eneo hilo.
Akizungumza na mkandarasi anayetekeleza mradi huo, Kanali Ngayalina amemtaka kuongeza juhudi na kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati uliopangwa, huku akisisitiza kuzingatia ubora wa kazi ili daraja hilo liweze kutoa huduma ya kudumu kwa wananchi.

Kukamilika, kwa daraja hilo kutarahisisha usafiri na usafirishaji kati ya vijiji vya Nyamihanga, Kirungu, Munzeze na Kishanga kuelekea Wilaya ya Kigoma na Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe, hivyo kuchochea biashara, huduma za kijamii na maendeleo ya wananchi kwa ujumla.