Radio Kwizera
Radio Kwizera
April 28, 2026, 1:06 pm

Wananchi wamehimizwa kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya, kutumia vyandarua vyenye viuatilifu pamoja na kudumisha usafi wa mazingira ili kupunguza mazalia ya mbu.
Na Shafiru Yusuph- Muleba, KAGERA
Wakazi wa Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera wametakiwa kuondoa mitazamo hasi pindi wanapopata dalili za ugonjwa wa malaria na badala yake kufika mapema kwenye vituo vya afya kwa ajili ya uchunguzi na matibabu sahihi.
Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Muleba Bw. Evart Kagaruki ambaye amemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Muleba amesema hayo kwenye maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani ambayo ki Wilaya yamefanyika Kata ya Kyebitembe kijiji cha Kasindaga.
Bw. Kagaruki amesema kuwa kuchelewa kutafuta matibabu kunachangia kuongezeka kwa madhara ya ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na vifo vinavyoweza kuzuilika.
Aidha, wananchi wamehimizwa kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya, kutumia vyandarua vyenye viuatilifu pamoja na kudumisha usafi wa mazingira ili kupunguza mazalia ya mbu.