Radio Kwizera

Wanawake FPCT Kakonko waanzisha mradi wa nyumba ya kupangisha

April 20, 2026, 7:01 pm

Baadhi ya Wanawake wa Kanisa la FPCT Kakonko walioshiriki sikukuu yao iliyoambatana na utambulisho wa mradi wa nyumba ya kupangisha walioanzisha. Picha na Samwel Masunzu

Mradi huo utagharimu shilingi milioni 10 ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuongeza kipato chao ndani ya kanisa ambapo mradi umefikia hatua ya msingi.

Na Samwel Masunzu- Kakonko, KIGOMA

Wanawake katika kanisa la Free Pentecostal Church FPCT Kakonko mjini mkoani Kigoma wameanzisha mradi wa nyumba ya kupangisha utakaowawezesha kuongeza kipato

Akisoma risla ya umoja wa wanawake hao UWW, Katibu wa wanawake wa Kanisa hilo Mercy Prosper amesema mradi huo utagharimu shilingi milioni 10 ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuongeza kipato chao ndani ya kanisa ambapo mradi umefikia hatua ya msingi.

Redio Kwizera imezungumza na Mwenyekiti wa UWW, Evelyn Erasto ambaye amesema mradi wa nyumba hiyo utawawezesha kupata shilingi laki 2 kila mwezi

Mgeni rasmi katika sherehe hiyo ya wanawake Afisa Elimu Idara ya Msingi Kakonko Bi. Isabella Mwakabonga akiendesha harambee ya kuchagia ujenzi huo, amewataka wanawake hao kutokujihusisha na migogoro wakati wa usimamizi wa mradi huo kabla na baada ya kukamilika.

Sikukuu ya wanawake katika Kanisa hilo imetanguliwa na shughuli mbalimbali tangu April 16 na kutamatika Aprili 19 ambapo usimamizi wa ibada na huduma nyingine umefanyika chini ya wanawake.

Naye mchungaji wa kanisa hilo Mathias Ndabunganiye amewapongeza wanawake kwa jitihada zao za kufanikisha shughuli hiyo pamoja na wale ambao wameweza kuwaunga mkono