FM Manyara

DC Kaganda awaonya wanaoharibu miundombinu

19 February 2026, 1:55 pm

Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda amekemea tabia ya baadhi ya wananchi wasio na uzalendo ambao wamekuwa wakiharibu miundombinu makusudi na kupelekea wananchi kukosa huduma.

Na Mzidalfa Zaid

Kaganda amesema hayo katika Baraza maalum la madiwani la halmashauri ya wilaya  ya Babati lililokutana kupitisha makadirio ya bajeti ya mwaka 2026-2027, amesema kila mwananchi ana wajibu wa kulinda miundomninu ya serikali.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda

Hatua hiyo imekuja baada ya baadhi ya madiwani kulalamikia changamoto ya kutokamilika kwa baadhi ya miradi, ikiwemo maji, umeme na afya ambapo wameiomba serikali kushughulikia changamoto hiyo.

Sauti ya baadhi ya madiwani
picha ya baadhi ya madiwani
picha ya baadhi ya madiwani

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Babati John Noya, ameitaka tarura kuhakikisha bara bara zote zinazotengenezwa zinawekwa mitaro ili kuepuka changamoto ya bara bara kuharibika mara kwa mara.

sauti ya Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Babati John Noya

Aidha Naibu waziri, ofisi ya rais – menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora, mhe. Regina Qwaray amewataka viongozi kutumia misingi ya haki, uwajibikaji na usawa.

sauti ya Naibu waziri, ofisi ya rais – menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora, mhe. Regina Qwaray
picha ya Naibu waziri, ofisi ya rais – menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora, mhe. Regina Qwaray