FM Manyara

Manyara watakiwa kuwatumia mawakili wenye weledi

20 January 2026, 5:12 pm

Picha ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga pamoja na Mkurugenzi wa uratibu na huduma za ushauri kutoka  ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Neema Ringo wakisikiliza malalamiko ya mwananchi.

Wananchi  mkoani Manyara wametakiwa  kutumia mawakili na wanasheria wenye weledi  katika utatuzi wa kesi mbalimbali  ili  changamoto zao  zitatuliwe  kwa wakati.

Na Mzidalfa Zaid

Mkuu wa mkoa wa manyara Queen Sendiga, ameyasema hayo leo wakati  akizindua  kamati  ya ushauri wa kisheria ngazi ya mkoa na wilaya  na kliniki ya sheria bila malipo ambayo imefanyika wilayani hanang mkoani manyara na kuwataka wananchi  kutumia klinik  hiyo  kuelezea changamoto zao  za  kisheria.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa manyara Queen Sendiga

Kwa  upande wake mkurugenzi wa uratibu na huduma za ushauri kutoka  ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Neema Ringo, amesema  kamati hizi imeanza kufanya kazi kuanzia january 19  hadi january 25 ambapo amesema zaidi ya wanasheria 30  wapo wilayani hanang kutoa  huduma  ya  kisheria.

sauti ya mkurugenzi wa uratibu na huduma za ushauri kutoka  ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Neema Ringo

Mbunge wa jimbo la Hanang Asia Halamga amesema wilaya ya Hanang ni wilaya yenye changamoto kubwa ya migogoro ya ardhi , hivyo kupitia klinik hii wananchi wengi watapata msaada wa kisheria.

sauti ya Mbunge wa jimbo la Hanang Asia Halamga

Aidha, baadhi ya wananchi ambao wameudhuria klinik hiyo, wameishukuru serikali kwa kutoa msaada wa kisheria bure kwani klinik hiyo itasaidia kutatua changamoto zao.

sauti ya wananchi
picha ya baadhi ya wananchi waliohudhuria