FM Manyara

Kamati  ya ushauri wa kisheria Manyara kutoa msaada wa kisheria  bure

19 January 2026, 4:50 pm

Picha ya Mkurugenzi wa uratibu  na huduma za ushauri kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Neema Ringo

Wananchi mkoani Manyara wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kamati ya ushauri wa kisheria ngazi ya mkoa na wilaya na kliniki ya Sheria bila malipo itakayofanyika wilayani hanang mkoani Manyara.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa na Leo na Mkurugenzi wa uratibu  na huduma za ushauri kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Neema Ringo wakati akizungumza katika kipindi Cha mseto wa Leo kinachorushwa Fm Manyara redio.

Sauti ya Mkurugenzi wa uratibu  na huduma za ushauri kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Neema Ringo

Amesema kamati hizo zitakuwa za kudumu kwa Lengo la kusikiliza na kutatua changamoto za kisheria , ambapo amewataka wananchi wenye changamoto ya kisheria kuzitumia kamati hizo kupatiwa ufumbuzi.

Kwa upande wake  mwanasheria wa serikali mfawidhi kutoka  ofisi ya wakili mkuu wa serikali ambae pia  ni mwenyekiti wa kamati ya ushauri wa kisheria mkoa wa Manyara Lameck Butuntu amesema Lengo la kuunda kamati hizo ni kushughulikia kwa haraka malalamiko yanayotolewa na wananchi.

sauti ya mwanasheria wa serikali mfawidhi kutoka  ofisi ya wakili mkuu wa serikali ambae pia  ni mwenyekiti wa kamati ya ushauri wa kisheria mkoa wa Manyara Lameck Butuntu
picha ya mwanasheria wa serikali mfawidhi kutoka  ofisi ya wakili mkuu wa serikali ambae pia  ni mwenyekiti wa kamati ya ushauri wa kisheria mkoa wa Manyara Lameck Butuntu

Nae  mkuu wa kitengo cha Sheria ofisi ya mkuu wa mkoa wa Manyara ambae ni katibu wa kamati ya ushauri wa kisheria mkoa wa Manyara Neema Gasabile amesema ofisi ya mkuu wa mkoa imekuwa ikipokea kesi nyingi , hivyo kupitia kamati hiyo malalamiko hayo yatatatuliwa kwa wakati.

sauti ya mkuu wa kitengo cha Sheria ofisi ya mkuu wa mkoa wa Manyara ambae ni katibu wa kamati ya ushauri wa kisheria mkoa wa Manyara Neema Gasabile
picha ya mkuu wa kitengo cha Sheria ofisi ya mkuu wa mkoa wa Manyara ambae ni katibu wa kamati ya ushauri wa kisheria mkoa wa Manyara Neema Gasabile

Aidha , uzinduzi wa kamati hiyo utafanyika katika viwanja vya mount hanang wilayani hanang na mgeni rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga na huduma ya kisheria imeanza kutolewa Leo January 19 hadi January 25.

picha ya mkurugenzi msaidizi uratibu na huduma za ushauri kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali