FM Manyara

Halmashauri ya mji wa Babati  yatoa tuzo kwa shule zilizofanya vizuri

4 December 2025, 2:13 pm

Picha ya baadhi ya wawakilishi wa shule katika mji wa Babati

Halmashauri ya mji wa  Babati  mkoani Manyara imetoa tuzo na zawadi kwa walimu na shule zilizofanya vizuri katika ufaulu wa masomo  .

Na Angel Munua

Hafla hiyo imefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa  ikiwa na lengo la kutoa hamasa kwa walimu ambao wamefanya vizuri katika masomo yao ambapo afisa elimu halmashauri ya wilaya ya Babati Simoni Mumbe amewapongeza walimu  kwa kazi kubwa wanavyofanya na kuhakikisha ufaulu unaongezeka .

Sauti ya afisa elimu halmashauri ya wilaya ya Babati Simoni Mumbe

Kwa upande wake mgeni rasmi ambaye ni mbunge wa Babati mjini Emmanuel Kambai amewapongeza walimu kwa kuongeza ufaulu ambapo ameahidi kushirikiana vizuri na wadau waelimu ili kutengeneza maz ingira rafiki ya ufaulu kwa wanafunzi.

Sauti ya mbunge wa Babati mjini Emmanuel Kambai
picha ya Sauti ya mbunge wa Babati mjini Emmanuel Kambai

Aidha kwa upande wa walimu ambao wamepata tuzo na zawadi kwa kufanya vizuri katika masomo yao wameishukuru halmashauri hiyo kwa kuandaa jambo hilo kwani limewatia hamasa ya kuzidi kufundisha kwa bidii .

sauti ya walimu