FM Manyara

Maafisa usafirishaji Manyara walalamikia mafuta kuadimika

4 November 2025, 5:04 pm

picha ya maafisa usafirishaji manyara

Maafisa usafirishaji  wilayani Babati mkoani Manyara wamelalamikia kuadimika kwa mafuta katika vituo vya kuuzia mafuta na kuiomba Serikali kuingilia kati suala hilo ili kurahisisha shughuli za uchumi kwa wananchi.

Na Marino Kawishe

Wakizungumza na fm Manyara wamesema, kituo kinachouza mafuta ni kimoja hali inayosababisha kuwepo kwa foleni ya kupata huduma hiyo, ambapo wanalazimika kupandisha bei ya nauli.

Sauti ya maafisa usafirishaji

Kufuatia changamoto hiyo  Fm Manyara imemtafuta katibu mkuu wa Latra CCC mkoani Manyara Claudina Haule amesema baadhi  ya madereva wamekuwa wakipandisha nauli kiholela wakati  huu  wa changamoto ya usafiri mkoani Manyara jambo ambalo ni kinyume na taratibu zilizowekwa na Mamlaka husika, amesema watachukua hatua za kisheria kwa madereva watakaobainika kwenda kinyume na sheria zilizowekwa na latra.

sauti ya katibu mkuu wa Latra CCC mkoani Manyara Claudina Haule