FM Manyara

Wananchi watakiwa kuiombea Nchi amani

27 October 2025, 12:01 pm

Picha ya Waziri mkuu Mstaafu Frederick Sumaye akisalimiana na wananchi wa kata ya Bashnet

Watanzania kote Nchini wametakiwa kuendelea kuliombea taifa Wakati huu Nchi ikielekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge  na Madiwani unaotarajiwa kufanyika October 29 mwaka huu.

Akizungumza na Wananchi waliojitokeza kwenye mkutano maalumu wa maombi wakuliombea taifa uliofanyika katika kata  ya Bashnet jimbo la Babati  Vijijini mkoani Manyara Waziri mkuu Mstaafu Frederick Sumaye amesema umoja na ushirikiano miongoni mwa Watanzania unatakiwa bila kubagua kabila la mtu.

Sauti ya Waziri mkuu Mstaafu Frederick Sumaye

Kwa upande wake mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM jimbo la Babati Vijijini na naibu waziri wa Mambo ya ndani  Daniel Baran Sillo amewata wananchi kuombea aman kabla ya uchaguzi  wakati wa uchaguzi na baada ya Uchaguzi….

Sauti ya mgombea ubunge jimbo la Babati vijijini

Mkutano huo maalumu wakuombea amani ya Nchi kabla ya uchaguzi umehudhuriwa na badhi ya  viongozi wa kidini pamoja na mila kutoka simanjiro, kiteto, Hanang na Halmashauri ya Babati Vijijini.

Picha ya mgombea ubunge jimbo la baba babati vijijini Baniel Baran Sillo akisalimiana na wananchi wa kata ya Bashnet