FM Manyara

Waziri Sumaye amnadi Sillo kabla ya October 29, 2025

24 October 2025, 12:35 am

Picha ya waziri mkuu Mstaafu Fredrick akimnadi Mgombea ubunge jimbo la Babati vijijini Daniel Sillo

Zikiwa zimesalia siku tano kabla ya uchaguzi mkuu wa kumchagua Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika October 29 mwaka huu hapa Nchini, Watanzania wamehimizwa kujitokeza na kupiga kura kwa wingi.

Na Marino Kawishe

Akizungumza na wananchi wa kata ya Ayalagala  Mratibu wa kampeni kwa Kanda ya Kaskazini Na waziri mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye amesema zipo ahadi ambazo zimetajwa na mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dr Samia Suluhu Hassan ambazo zitafanyiwa kazi kwa siku mia moja iwapo atashinda.

Sauti ya waziri mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye

Naye Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi jimbo la uchaguzi la Babati Vijijini Daniel Baran Sillo amesema vipaumbele vyake vyote alivyoahidi kwenye kampeni atavipa msukumo mkubwa  kwasababu analo deni la kuwalipa wapiga kura wake.

Sauti ya mkombea ubunge jimbo la Babati Vijijini Daniel Baran Sillo

Aidha Sillo amesema ni kweli hana mpinzani lakini hilo halitoshi kusema ameshinda  lazima wananchi kujitokeza kupiga kura ya ndio ili aweze kushinda na kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa kipindi kingine cha miaka mitano ijayo.