FM Manyara

Sillo ahaidi kukamilisha miradi iliyosalia Magara

21 October 2025, 11:13 pm

Picha ya Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM jimbo la uchaguzi la Babati Vijijini Danieli Baran Sillo

Na Marino Kawishe

Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM jimbo la uchaguzi la Babati Vijijini Danieli Baran Sillo ameendelea kunadi ilani ya chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu  unaotarajiwa kufanyika  October 29, kwa wananchi wa kata ya Magara na Mwada kwa kuhaidi kukamilisha miradi  mbali mbali iliyoanzishwa kwa miaka mitano iliyopita.

Akihutubia wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni Mgombea ubunge wa jimbo hilo Daniel Baran Sillo amesema tatizo la kutokuwepo kwa maji safi na salama pamoja na umeme kwa baadhi ya Vitongoji ameyapokea na atayafanyia kazi  baada ya kupata ridhaa yakuchaguliwa na wananchi  kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Nchini  October 29.

Kwa upande wake Mgombea udiwan wa kata ya Magara Gonzalez Mkoma amemuomba Mgombea ubunge Wa Jimbo la Babati Vijijini  kukamilisha changamoto hizo na kuomba wananchi kumchagua kwa kura ya ndio ili aweze kusaidiana na mbunge kukamilisha miradi hiyo.

Mgombea ubunge huyo anatarajia kuendelea na mikutano ya kampeni hapo kesho  October  22 kwenye kata ya magugu na kiru.