FM Manyara

Manyara watakiwa kuongeza thamani ya mbogamboga, mikunde

9 October 2025, 9:48 pm

Picha ya baadhi ya wafanyabiashara wakipatiwa mafunzo

Wakulima mkoani Manyara wametakiwa kuongeza thamani ya mazao ya mbogamboga na mikunde kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali zinazotokana na mazao hayo  ili kupata masoko ya uhakika ya ndani na nje ya nchi badala ya kuuza mazao ghafi kwa bei ya chini.

Na Mzialfa Zaid

Akizungumza katika mafunzo  ya kuongeza thamani ya mazao ya mbogamboga na mikunde yaliyoandaliwa na Shirika la World Vegetable Center kwa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara pamoja na Sido, Kaim Katibu tawala mkoa wa Manyara Faraja Ngerageza amesema itasaidia kuongeza thamani ya mazao yanayopatikana  ndani ya mkoa wa Manyara.

Sauti ya kaimu Katibu Tawala mkoa wa Manyara
Picha ya kaim katibu tawala mkoa wa Manyara

Kwa upande wake Mtafiti Mwandamizi wa kitengo cha uchumi jamii kutoka Shirika la World Vegetable Center Inviolate Dominick amesema mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha wakulima wanaotengeneza bidhaa mbali mbali kutokana na mboga mboga na mikunde.

Sauti ya Mtafiti Mwandamizi wa kitengo cha uchumi jamii kutoka Shirika la World Vegetable Center Inviolate Dominick
Picha ya Mtafiti Mwandamizi wa kitengo cha uchumi jamii kutoka Shirika la World Vegetable Center Inviolate Dominick

 Meneja wa Sido mkoa wa Manyara Abel Mapunda amewataka wananchi mkoani Manyara kufika Sido ili wajifunze ujasiriamali tofauti utakaowasaidia kuwainua kiuchumi.

Sauti ya Meneja wa Sido mkoa wa Manyara Abel Mapunda
Picha ya Meneja wa Sido mkoa wa Manyara Abel Mapunda

Afisa biashara wa mkoa wa manyara Ally Mokiwa amesema mafunzo hayo yatawasaidia wafanyabiashara kuinua kipato chao kupitia ubunifu.

Sauti ya Afisa biashara wa mkoa wa manyara Ally Mokiwa
Picha ya Afisa biashara wa mkoa wa manyara Ally Mokiwa

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamesema mafunzo hayo yatawasaidia kiuchumi  kuongezewa thamani.

Sauti ya washiriki
Picha ya baadhi ya washiriki