FM Manyara

Wazazi watakiwa kuwekeza elimu kwa watoto

30 September 2025, 7:16 pm

Picha ya mkurugenzi mkuu wa shule za Amka Africa na Angaza Manyara Bw.Simon Msangi kulia akuwa na Mkurugenzi mkuu Ruwasa Nchini Wolter Kirita katikati.

Na Marino Kawishe

 Wazazi na Walezi wamehimizwa kutokuchoka kujinyima na kuwekeza kwa watoto wao ili wapate elimu bora itakayowasaidia kuchangamkia fursa mbali mbali  wanapokuwa wamehitimu mafunzo yao.

Akizungumza na wananchi mkoani Manyara kwenye mahafali ya kumi ya shule ya Amka Africa Mkurugenzi mkuu wa Ruwasa hapa nchini  Wolter Kirita amesema kwa ulimwengu wa sasa zawadi kubwa itakayomsaidia mwanafunzi kwenye maisha yake ni elimu.

Sauti ya Mkurugenzi mkuu Ruwasa nchini Tanzania

Kwa upande wake Mkurugenzi  mkuu wa Shule za Amka Africa na Angaza Manyara zilizopo mjini Babati Simon Msangi amesema wanafurahi kuona wazazi wanaendeleza ushirikiano baina yao na waalimu na sasa wameanza kufundisha somo la Kichina shuleni hapo somo ambalo linapendwa zaidi na wanafunzi.

Sauti ya Mkurugenzi  mkuu wa Shule za Amka Africa

Aidha uongozi wa shule hizo umekiri ongezeko la wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo ambapo sasa wana zaidi ya wanafunzi elfu moja na mia nne, na kutoa fursa ya kuanza upanuzi wa miundo mbinu ya madarasa mapya.

Na katika kuunga mkono hilo mfanyabiashara maarufu mjini babati maarufu Mama Hango amechangia kiasi cha sh milion moja ili kuwezesha mipango hiyo kukamilika.

Mgeni rasmi Wolter Kirita akitoa vyeti kwa wahitimu wa darasa la saba shule ya msingi Amka Africa na Angaza Manyara waliofanya vizuri katika masomo yao.