FM Manyara

Ndege amnadi mgombea udiwani Riroda

25 September 2025, 9:45 am

Picha ya mgeni Rasmi katika mkutano wa kampeni za udiwani kata Riroda kijiji cha Sangara Rejina Ndege akimnadi mgombea Udiwani wa kata hiyo Nyangweli Bombo kupitia chama cha Mapinduzi.

Na Marino Kawishe

Kuelekea uchaguzi mkuu  wa Rais,Wabunge na Madiwani  unaotarajiwa kufanyika October 29 mwaka huu hapa Nchini Wananchi wa kata ya Riroda wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura wakiwa na kadi za mpiga kura ili kumchagua Rais Samia Suluhu Hasan.

Akifungua kampeni za mgombea Udiwani wa kata ya Riroda kwa tiketi ya CCM mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara Regina Ndege  amesema uchaguzi ujao ni muhimu kwa Wananchi  na hasa kumchagua mgombea Udiwani huyo ambaye ataziwasilisha kero mbali mbali za wananchi wa kata hiyo kwa mbunge ili zitatuliwe.

Mbunge Mteule wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara Regina Ndege 

Kwa upande wake mwenyekiti Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa  Manyara  Janes Darabe amewataka wananchi kutumia kura yao kwa Rais Dr Samia Suluhu, Mbunge wa jimbo la Babati Vijijini na Kwa diwani kwa kumpa kura ya ndio.

Sauti ya Mwenyekiti Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa  Manyara  Janes Darabe

Aidha mgombea Udiwani wa kata ya Riroda  Nyangweli Bombo amesema akichaguliwa kwa kura za ndio kwenye uchaguzi huo atahakikisha kijiji cha Sangara kinajengwa Zahanati itakayotumika kutoa huduma za afya kwa Wananchi wa Kijiji hicho.

Wananchi wa kijiji cha Sangara Kata ya Riroda wakisikiliza sera za mgombea wa udiwani wa kata hiyo kupitia chama cha Mapinduzi