FM Manyara

Asia Halamga azindua kampeni Hanang’

16 September 2025, 4:36 pm

Picha ya mgombea wa jimbo la hanang’ Asia Halamga akinadi sera zake mbele ya wananchi wa kata ya gehandu.

Na Marino Kawishe

Wananchi katika jimbo  la hanang mkoani manyara wametakiwa kujitokeza october 29 kwenye uchaguzi mkuu wakumchagua rais, wabunge  na madiwani.

Akifungua kampeni za kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la hanang kwa tiketi ya ccm, mjumbe wa mkutano mkuu taifa ccm Namelock Sokoine, amesema haoni sababu ya wananchi kushindwa kujitokeza kumchagua rais  dkt Samia na Asia Halamga  kama mbunge wao kwa kuwa  mambo mengi yamefanywa Hanang kwa miaka 4 ya uongozi wa Rais  dkt samia Suluhu Hassan.

Sauti ya mjumbe wa mkutano mkuu taifa ccm Namelock Sokoine

Kwa upande wake mbunge anayewania ubunge jimbo hilo kwa tiketi ya ccm Asia Halamga amesema  vipaumbele vyake muhimu ambavyo atavisemea bungeni iwapo atapata ridhaa ya wana-hanang october 29 kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka  2025.

Sauti ya mgombea ubunge jimbo la Hanang’ Asia Halamga

Katika ufunguzi huo wa kampeni katika jimbo la uchaguzi la Hanang umehudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye ambaye amesema wananchi wanapaswa kutumia tarehe ya uchaguzi kumchagua rais  dkt Samia Suluhu Hasan, mbunge na madiwani wote 33 katika jimbo hilo.

Picha ya wananchi wa kata ya Gehandu wakiwa katika kampeni za mgombea Ubunge jimbo la Hanang’