FM Manyara

Maafisa mifugo Babati Mji wakabidhiwa vishikwambi

15 September 2025, 6:29 pm

Picha ya Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Babati Shaaban Mpendu na maafisa mifugo

Mkurugenzi wa halmashauri ya mji Babati CPA. Shaaban Mpendu  amekabidhi vishikwambi kwa wataalam wa mifugo na kuwaasa kutunza na kutumia vishikwambi hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa.

Na Mzidalfa Zaid

Amesema vishikwambi hivyo vimetolewa na serikali kupitia wizara ya mifugo na uvuvi, ambapo jumla ya vishikwambi 12 vimetolewa ili kuongeza ufanisi na kuwezesha utoaji wa taarifa ya chanjo na utambuzi pamoja na kuingiza taarifa kwenye mfumo wa utambuzi na usajili katika zoezi la chanjo linaloendelea kitaifa.

Sauti ya Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Babati Shaaban Mpendu
Picha ya Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Babati Shaaban Mpendu

Kwa upande wake Daktari wa mifugo na mratibu wa chanjo halmashauri ya mji wa Babati Fatuma Mkombozi amesema  hadi sasa wamefikia 62% ya uchanjaji kwa ng’ombe, 89% upande wa kuku, na 33.7% kwa mbuzi na kondoo.

Sauti ya Daktari wa mifugo Fatuma Mkombozi

Nao baadhi ya maafisa mifugo wa kata mbalibali za halmashauri ya mji wa Babati ambao wamekabidhiwa vishikwambi hivyo, wamesema vitawasaidia kurahisha utendaji kazi.

Sauti za maafisa mifugo
Picha ya maafisa mifugo

Aidha, zoezi la chanjo kwa mifugo lilianza tarehe 24 julai 2025 kwa upande wa kuku na agosti 20 2025 kwa ng’ombe,mbuzi na kondoo.