FM Manyara

Sillo azindua kampeni za Ubunge Babati vijijini kwa kishindo.

12 September 2025, 10:32 am

Mgombea nafasi ya ubunge jimbo la Babati vijijini Daniel Sillo akinadi sera zake kwa Wananchi wa kata ya Mamire wilayani Babati

Na Marino Kawishe

Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi ( CCM) jimbo la Babati Vijijini Daniel Baran Sillo amewataka wananchi wa jimbo la Babati Vijijini kumchagua Rais Dr Samia Suluh Hassan kwenye uchaguzi utakaofanyika tarehe 29 october mwaka huu.

Akizungumza mbele ya wananchi wa kata ya Mamire waliohudhuria ufunguzi wa kampeni zake amesema vipaumbele vyake atakapopata nafasi yakuwa Mbunge wa jimbo hilo  kwa awamu nyingine ni kuhakikisha miundo mbinu ya barabara, elimu, upatikanaji wa maji  safi na salama na huduma za afya ambayo ilishaanza wakati akiwa mbunge  inakamilika ili kutatua kero kwa wananchi wa jimbo lake.

Sauti ya mgombea ubunge (ccm) jimbo la Babati vijijini

Kwa upande wake Mgeni Rasmi kwenye uzinduzi wa kampeni hizo  ambaye ni mjumbe wa mkutano Mkuu  CCM Taifa Joachim Muungano amemuomba aliyekuwa Diwani wa kata ya Mamire Tarmo Kurudi ndani ya chama chake cha CCM ili kukamilisha kwa pamoja miradi ambayo ilishaanzishwa wakati akiwa Diwani wa kata hiyo

Aidha aliyekuwa  mtia  nia wa kuwania ubunge katika jimbo la Babati Vijijini Emanuel Philip Gekul ambaye hakufanikiwa kuchaguliwa wakati wa kura za maoni amewataka Wana CCM kutokuwa na Makundi na badala yake kumuunga mkono Daniel Sillo pamoja na madiwani waliopitishwa kwa tiketi ya CCM kwenye uchaguzi ujao.

Sauti ya MNEC na aliyegombea ubunge jimbo la Babati vijijini

Katika ufunguzi huo wa Kampeni za mgombea  ubunge wa jimbo la Babati Vijijini zimehudhuriwa na wagombea udiwani wote  wa kata 25 pamoja na Baadhi ya wagombea wa nafasi ya ubunge akiwemo Asia Halamga kutoka Hanang na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara Regina Ndege.