FM Manyara

Mkungunero na fursa za uwekezaji kufuga wanyamapori

1 September 2025, 4:18 pm

Picha ya baadhi ya viongozi kutoka pori la akiba Mkungunero

Wawekezaji  mkoani Manyara wanaohitaji kufuga wanyamapori na kuwapa fursa wananchi kuona wanyama katika maeneo yao, wametakiwa kuwasiliana na uongozi wa  pori la akiba Mkungunero ili kupewa utaratibu wa kufuga wanyama hao.

Na Mzidalfa Zaid

Hayo yameelezewa leo na afisa Utalii pori la akiba Mkungunero Wilfred Kilonzo wakati akiongea na Fm Manyara, amesema wanatoa fursa kwa wananchi kujiinua kiuchumi kupitia pori hilo kwa kuwafuga wanyama wanaoishi katika hifadhi kwenye maeneo yao.

Sauti ya afisa Utalii pori la akiba Mkungunero Wilfred Kilonzo

Kwa upande wake Afisa Mhifadhi Pori la akiba Mkungunero Tumain Minja, amesema kumekuwepo na changamoto ya wanyama kuvamia makazi ya watu, ambapo amewataka wananchi kutumia njia zinazotolewa na wataalamu kudhibiti wanyama hao wakiwemo tembo.

Sauti ya Afisa Mhifadhi Pori la akiba Mkungunero Tumain Minja