FM Manyara

   Dereva afariki kwa ajali ya gari babati

5 June 2025, 7:00 pm

Usanifu mbovu wa daraja lililopo kati ya kijiji cha majengo na orongadida wilayani babati umekuwa chanzo cha ajali nyingi kutokea katika daraja hilo.

Na George Augustino.

kijana aliyefahamika kwa jina moja maarufu la digidigi (48) amefariki dunia katika ajali ya gari la mizigo iliyotokea leo majira ya saa tano asubuhi katika daraja linalounganisha kijiji cha orongadida na kijiji cha majengo vilivyopo katika kata ya qash wilayani babati mkoani manyara .

akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo mwenyekiti wa kijiji cha majengo saruni meliari amesema ajali hiyo imetokea baada ya gari hilo  lililokuwa limebeba mizigo ya wafanyabiashara wa mnada kutokea kijiji cha gallapo kufeli breki na kuangukiw katika korongo hilo na kumuua dereva aliyekuwa akiliendesha gari hilo.

Sauti ya mwenyekiti wa kijiji cha Majengo

kwa upande wao wananchi na wafanyabiashara waliokuwa wakisafiri na gari hilo wameiomba serikali kuwasaidia kurekebisha na kujenga upya daraja hilo ambalo limekuwa likisababisha vifo vya watu wengi ambao ni nguvu kazi ya taifa.

Sauti za mashughuda wa ajali