FM Manyara

CSP  yaadhimisha Siku  ya Mazingira Duniani kwa kutoa elimu

5 June 2025, 6:32 pm

Kila tarehe 5 Juni, kila mwaka Watanzania tunaungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani kwa kufanya shughuli mbalimbali za kimazingira ikiwemo usafi wa mazingira na upandaji wa miti.

Na George Augustino

shirika lisilo la serikali la civil social protection lililopo wilayani babati mkoani manyara limeadhimisha  siku ya mazingira duniani leo kwa kufanya usafi katika maeneo ya shule ya msingi  darajani na katika eneo la mtaa wa maisaka b mjini babati mkoani manyara.

akizungumza na fm manyara wakati wa zoezi hilo afisa programu  upande wa mazingira wa shirika hilo eliakim warikoi amesema wameamua kuadhimisha siku hii ili  kuihamasisha jamii kuendelea kufanya usafi na kutunza mazingira pamoja na kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira katika jamii na taasisi mbalimbali.

Sauti ya afisa programu  upande wa mazingira wa shirika la ulinzi wa jamii

kwa upande wao baadhi ya wananchi wa mtaa wa maisaka b wamesema  wamehamasika kushiriki katika kufanya usafi wa mazingira pamoja na shirika hillo katika mtaa wao kwakuwa usafi wa mazingira ni muhimu kwaajili ya kulinda  afya zao kutokana na magonjwa ya mlipuko.

Sauti za wananchi wa mtaa wa maisaka B

Aidha,mwalimu wa mazingira pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi darajani wamelishukuru shirika hilo la ulinzi wa jamii kwa kuwapa elimu ya utunzaji wa  mazingira nakusema  elimu hiyo wataitumia hata watakapokuwa majumbani.

Sauti ya Mwalimu na Wanafunzi

Kaulimbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira mwaka huu 2025 kitaifa ni “Mkaa Gharama; Tumia Nishati Mbadala”