FM Manyara

Jamii Manyara yatakiwa kusaidia wasichana shuleni kupata taulo za kike

8 May 2025, 5:51 pm

Suala la hedhi salama lina mchango mkubwa katika kupunguza utoro ambapo
Jamii mkoani Manyara imetakiwa kuunganisha nguvu za pamoja katika kusaidia wasichana shuleni ili kupata taulo za kike

Na Mzidalifa Zaid

Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Maryam  Ahmed  Muhaji ameitaka jamii kuunganisha nguvu za pamoja katika kusaidia wasichana shuleni ili kupata taulo za kike katika kustawisha hedhi salama na kufanya vizuri katika masomo yao.

Muhaji ameyasema wilayani  Babati mkoani Manyara wakati wa mafunzo kwa  baadhi ya wanafunzi na walimu  pamoja na  wadau  wengine  wa  Afya   mkoani Manyara na ngazi ya taifa kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi  ya taulo za kike na utambulisho wa  mradi wa usambazaji wa taulo za kike  kutoka Kampuni ya Real Relief kupitia mradi wa SAFEPAD na kampuni ya A to Z.

sauti ya Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Maryam  Ahmed  Muhaji

Kwa upande wake Afisa  Programu kutoka Mpango wa Taifa wa Afya na Lishe Shuleni , Wizara ya Afya Dkt. Julietha Tibyesiga amesema hedhi salama inapozingatiwa ni namna bora ya kumtunza  msichana shuleni ili aweze kusoma vizuri na akizungumzia Maandalizi ya Mwongozo wa  Usimamizi wa Hedhi salama.

sauti ya Afisa  Programu kutoka Mpango wa Taifa wa Afya na Lishe Shuleni , Wizara ya Afya Dkt. Julietha Tibyesiga

Katibu wa Jukwaa la Hedhi Salama Tanzania  Severine Allute na Irine Maganga kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wamesema mradi wa SAFEPAD utarahisisha wanafunzi kuwa na mazingira safi na salama na kuwezesha kujifunza kwa ufasaha na mradi huo utarahisisha Mkoa wa Manyara kuwa na upatikanaji wa taulo za kike.

sauti ya Katibu wa Jukwaa la Hedhi Salama Tanzania  Severine Allute
sauti ya Irine Maganga kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Nao baadhi ya wanafunzi wanufaika wamradi huo  akiwemo Zaina  Khatibu kutoka shule ya Sekondari Babati Day pamoja na Anna Bahati kutoka shule ya Msingi Komoto wamesema suala la hedhi salama lina mchango mkubwa katika kupunguza utoro shuleni na wakishukuru mafunzo yaliyotolewa kupitia mradi huo.

sauti ya wanafunzi