FM Manyara

Madaktari bingwa 45 wawasili Manyara

24 September 2024, 11:15 am

Picha ya mkuu wa wilaya ya babati Emmanuela Kaganda akiwa amekaa katikati ya viongozi wengine wa hospitali na madaktari bingwa waliowasili mkoa wa manyara kutoa huduma za kibingwa

Mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kagandaamewataka wananchi mkoani Manyara kutumia fursa za matibabu zinazotolewa na madaktari bingwa bobezi 45 pamoja na wataalamu  wa afya 27 kutoka wizara ya afya  kwa muda wa siku sita.

Na George Augustino

Wananchi mkoani Manyara wametakiwa kujitokeza kupata huduma za matibabu katika hospitali zote za halmashauri  ya mkoa wa Manyara ambapo huduma hizo zinatolewa  na madaktari bingwa bobezi wa magonjwa mbali mbali   kutoka wizara ya afya  kuanzia septemba 23 hadi septemba 27 mwaka huu

Akizungumza katika hafla ya kuwapokea madaktari hao bingwa nabobezi katika hospitali ya mji wa Babati mrara mkuu wa wilaya ya Babati Emmanuela Kaganda ambaye amemuwakilisha mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga, amewataka wananchi mkoani Manyara kutumia fursa hiyo ya matibabu ambapo huduma hiyo itatolewa kwa muda wa siku sita na madaktari 45 pamona na wataalamu wengine wa afya

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Babati

kwa upande wake mganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa Manyara  Andrew method lyaruu amemshukuru Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania  Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kuwaleta madaktari bingwa bobezi katika mkoa wa Manyara na ameahidi kutoa ushirikiano kwa madaktari  hao ili wananchi watakofika wapate huduma kwa wakati unaotakiwa.

Sauti ya Mganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa Manyara

Aidha baadhi ya wananchi waliofika kupata huduma hizo wameshukuru ujio wa madaktari  hao na kuiomba serikali kuendelea kutoa huduma hizo mara kwa mara katika mikoa ili kuwafikia wananchi wote kwa urahisi na kupunguza gharama za matibabu.

Sauti za wananchi