FM Manyara

Polisi Manyara yakamata watuhumiwa 50 wa uhalifu

July 18, 2024, 2:03 pm

Picha ya kamanda wa polisi mkoa wa Manyara George Katabazi

Jeshi la polisi mkoani Manyara limewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kufichua wahalifu wa makosa ya ukatili wa kingono, dawa za kulevya na umiliki wa silaha kinyume na sheria  ili mkoa uendele kuwa salama.

Na Angela Munuo

Jeshi  la polisi mkoani Manyara  limesema katika kipindi cha kuanzia mwezi january hadi julai 2024 wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 50 waliohusika katika matukio mbali mbali ya uhalifu ikiwemo  wizi na ukatili kwa kijinsia ambapo washtakiwa 13 wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na washtakiwa 7 wamefungwa kifungo cha maisha .

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara George katabazi ameyasema hayo julay 17alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, amesema katika operesheni hiyo wamefanikiwa kukamata silaha nne ambazo ni pisto mbili pamoja na magobore mawili ambazo zilikuwa zikimilikiwa kinyume cha sheria .

Sauti ya kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara

 Kamanda Katabazi amesema jeshi la polisi katika operesheni zake wamefanikiwa  kukamata pikipiki sitini na tano ( 65) zinazozaniwa ni mali ya wizi pamoja na watuhumiwa (25) wa makosa ya wizi nakusema katika kesi za ukatili wa kingono  washtakiwa saba wamehukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la kulawiti na kubaka watoto wenye umri kati ya miaka 5-14 na wengine 13 wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela.

Sauti ya kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara

Aidha  Kamanda Katabazi amewataka wananchi  mkoani Manyara kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kufichua wahalifu wa makosa ya ukatili wa kingono, dawa za kulevya na umiliki wa silaha kinyume na sheria  ili mkoa uendele kuwa salama.