FM Manyara

Ubakaji, ulawiti vyashamiri Manyara

June 18, 2024, 7:25 pm

Picha ya Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Halmashauri ya Mji wa Babati Dianna Mchonga akitoa elimu kwa wanafunzi

Katika kukomesha vitendo vya ukatili kwa watoto mkoani Manyara jamii yatakiwa kuwapa elimu watoto wao kwakua  kufanya hivyo kutawasaidia watoto hao kupambanana na kila aina ya ukatili.

Na Marino Kawishe

Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mji Babati  imetoa ripoti ya mwenendo wa hali ya ukatili  wilayani  Babati mkoani Manyara tangu Januari hadi mwezi Juni kwa mwaka 2024 ambapo  vitendo vya ulawiti na ubakaji kwa watoto vinatajwa kuchukua nafasi kubwa katika jamii.

Akisoma ripoti hiyo mbele ya wananchi wa kata ya Bonga waliojitokeza kwenye maadhimisho ya siku ya  mtoto wa Africa ambayo yemefanyika  shule ya msingi Bonga  mkuu wa idara ya Maendeleo Halmashauri ya mji  wa Babati  Diana mchonga amesema juhudi zinahitajika ili kutokomeza vitendo hivyo.

Sauti yamkuu wa idara ya maendeleo Halmashauri ya mji wa Babati

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Babati, Abdurahaman Kololii amewataka wazazi na walezi kuwapa elimu watoto wao kwakua  kufanya hivyo kutawasaidia watoto hao kupambanana na kila aina ya ukatili.

Sauti ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Babati

Aidha, siku ya mtoto wa Africa huadhimishwa  kila ifikapo june 16 nakauli mbiu ya  mwaka huu  2024 inasema ELIMU JUMUISHI KWA WATOTO IZINGATIE MAARIFA , MAADILI NA STADI ZA KAZI’